Monday, November 11, 2013

Tanzanite yatua Dar kuivutia kasi Afrika Kusini

Timu ya Taifa Wanawake walio chini ya umri wa miaka 20 (Tanzanite)
Na John Dande, Dar es Salaam:     

TIMU ya Taifa ya Wanawake walio chini ya umri wa miaka 20 (Tanzanite), imefuzu kucheza raundi ya pili ya michuano ya Kombe la Dunia kwa ushindi wa jumla ya mabao 15-1, baada ya juzi kuinyuka Msumbiji mabao 5-1.

Mabao ya Tanzanite katika mechi hiyo iliyochezwa kwenye Uwanja wa Taifa wa Zimpeto jijini Maputo, yalifungwa na Sherida Boniface aliyepachika matatu (hat trick) wakati mengine yalifungwa na Vumilia Maarifa na Donesia Minja.

Msafara wa Tanzanite ulioongozwa na Mjumbe wa Kamati ya Utendaji ya Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Wilfred Kidao uliwasili jana alasiri Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA).

Akizungumza baada ya kuwasili nchini jana, kocha mkuu wa timu hiyo, Rogasian Kaijage alisema mechi ilikuwa ngumu lakini kwa sasa wanajipanga kuikabili Afrika Kusini katika mechi itakayochezwa kati ya Desemba 6 na 8 mwaka huu jijini Dar es Salaam.

0 comments:

Post a Comment